Thursday , 4 July 2024
Home Habari Mchanganyiko Mbowe: Tunawaunga mkono Kariakoo, mifumo ya kodi inaua mitaji
Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mbowe: Tunawaunga mkono Kariakoo, mifumo ya kodi inaua mitaji

Mbowe akihutubia Monduli
Spread the love

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amesema anawaunga mkono wafanyabiashara wa Kariakoo walioanza mgomo jana Jumatatu kuishinikiza serikali kutatua changamoto zao na kuwaomba wafanyabiashara wengine Tanzania nzima waungane na wenzao. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akihutubia wananchi na wafuasi wa chama hicho katika mkutano wa hadhara uliofanyika Monduli jana, Mbowe amesema inabidi wafanyabiashara hao waungwe mkono ili serikali ijue namna wananchi walivyo na hasira kutokana na ugumu wa maisha.

“Wafanyabiashara wa Kariakoo wanasema kodi zimekuwa kubwa, wananchi wanashindwa kununua bidhaa, Serikali ipunguze kodi tunaua mitaji yetu. Tunawaunga mkono wafanyabiashara wa Kariakoo, tunawaomba wafanyabiashara wengine Tanzania nzima tufike mahali tuikatae hii Serikali ya wahuni,” amesema Mbowe na kuongeza;

“Hasira za namna hii ndio hicho watoto wa Kenya wanachofanya. Wakati tozo ya simu na miamala inaanzishwa, Watanzania tuliangalia lakini Wakenya wanajitambua wameandamana  mpaka serikali imekubali kuondoa.

“Hii mijamaa inakopa sana kwa sababu zaidi ya asilimia 51 ya bajeti ya serikali ni kulipa madeni.  Hawana namna ya kuendesha serikali ndio maana lazima walete mzigo kwenu na hatujui fedha waliyokopa wamefanyia nini kwa sababu mikataba yote ya serikali ni siri… tumebaki kukopa Jumatatu mpaka Alhamisi,” amesema.

Amesema mifumo ya kodi inaua mitaji ya wafanyabiashara wengi na kusababisha ugumu wa maisha kwa watanzania.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Waingereza kuifuta historia ya Conservatives leo?

Spread the loveWaingereza milioni 50 wanatarajiwa kupiga kura kwenye uchaguzi mkuu leo...

Habari za SiasaKimataifa

Rais Biden agoma kujitoa uchaguzi Novemba, aangukia pua kura za maoni

Spread the loveRAIS wa Marekani, Joe Biden amekataa kujitoa kwenye uchaguzi wa...

BiasharaHabari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia, Nyusi wapongeza mkakati wa utanuzi PBZ, yakaribishwa kufungua tawi Msumbiji

Spread the loveRais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amepongeza jitihada zinazofanywa na...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Bwire Mtendaji mpya DAWASA

Spread the loveMhandisi Mkama Bwire ameteuliwa kushika nafasi ya Kaimu Afisa Mtendaji...

error: Content is protected !!