Sunday , 30 June 2024
Home Habari Mchanganyiko Madereva bodaboda wapewa ujumbe
Habari Mchanganyiko

Madereva bodaboda wapewa ujumbe

Spread the love

MADEREVA wawanaosafirirsha abiria kwa kutumia pikipiki (bodaboda), wametakiwa kuendelea kufanya shughuli zao kwa umakini kwa kuwa kazi hiyo ndiyo inayowapa riziki ya kuendesha maisha yao na familia zao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Wito huo umetolewa leo Jumatano na Mwanaharakati Bihimba Mpaya, wakati anakibidhi msaada wa pikipiki tatu kwenye kikundi cha Bodaboda Kivule, kilichopo jijini Dar es Salaam.

Bihimba ambaye ni mlezi wa kikundi hicho, amesema kuna baadhi ya bodaboda wamefanikiwa kujenga nyumba na kujikwamua kiuchumi kupitia kazi hiyo.

“Leo nikiongea na vijana wangu nilichowaambia wafanye kazi kwa bidii na kwa kifua mbele kwa kuwa ni bodaboda ni kazi kama zilivyo kazi zingine ndio maana vijana wameweza kupanga vyumba vya kuishi na familia zao Hadi wengine wamenunua viwanja na wanaanza kujenga,” amesema Bihimba.

Bihimba amesema ametoa msaada wa pikipiki hizo ili kuwasaidia  vijana wengine wasiokuwa nazo waweze kujiajiri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mpina amng’ang’ania Bashe, kumburuza mahakamani pamoja na bodi ya sukari

Spread the loveMbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amesema amenuia kumpeleka mahakamani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Majahazi yadakwa na madumu 1,731 ya mafuta ya kupikia

Spread the loveKikosi kazi cha Polisi Wanamaji Dar es Salaam kimekamata majahazi...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa wa mauaji ya mtoto mwenye ualbino wafikishwa mahakamani

Spread the loveWATUHUMIWA wa mauaji ya Asimwe Novath, mtoto mwenye ualbino, wamefikishwa...

Habari Mchanganyiko

Sangoma awaponza vijeba, watupwa jela maisha kwa kubaka wanafunzi

Spread the loveMAHAKAMA ya wilaya Nkasi Mkoani Rukwa, imemhukumu kifungo cha maisha...

error: Content is protected !!