Sunday , 30 June 2024
Home Habari Mchanganyiko CCM Igunga wanolewa kuhusu sheria usalama barabarani
Habari Mchanganyiko

CCM Igunga wanolewa kuhusu sheria usalama barabarani

Spread the love

Viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Igunga mkoani Tabora, waliogawiwa pikipiki kwa ajili ya shughuli za chama wilayani humo, wametakiwa kufuata sheria za usalama barabarani ili waepuke ajali za barabarani. Anaripoti Victor Makinda, Tabora … (endelea).

Hayo yameelezwa mjini Igunga na Askari wa  kikosi cha usalama barabarani, Koplo Josiah, wakati akitoa mafunzo ya usalama barabarani yaliyowahusisha wenyeviti, makatibu  wa CCM  wa Jumuiya zote za chama ngazi ya kata jimbo la uchaguzi Igunga.

Koplo Josiah aliwaeleza viongozi hao wa CCM kuzingatia sheria za usalama pindi wanapoendesha vyombo hivyo ili waweze kuepuka  kufanya makosa yatakayowasababishia ajali.

“Kujua tu kuendesha  chombo cha moto haitoshi, mnapaswa kuzijua na kuzifuata sheria zote za usalama barabarani ili muweze kuepuakana na ajali,” amesema Koplo Josiah.

Ameongeza kuwa kila mtu anayetumia chombo cha moto cha usafiri, anapaswa kuwa na leseni hai ya udereva na kuhakikisha kuwa chombo anachokitumia kimekatiwa bima.

Pia amewataka viongozi hao wa CCM ambao hawana leseni za udereva kuhudhuria mafunzo maalum ya udereva kwenye vyuo vya ufundi stadi (VETA).

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo Mbunge wa Igunga, Nicholaus Ngassa ambaye ndiye aliyeandaa mafunzo hayo kwa viongozi hao wa chama,  amesema kuwa jumla ya pikipiki 64 zimetolewa na CCM kwa viongozi wa kata 16 jimboni Igunga ili waweze kutekeleza majukumu yao..

Ngassa aliwaasa viongozi hao kuhakikisha kuwa wanafuata sheria za usalama barabarani ili waweze kuendesha kwa usalama na kutekeleza majukumu yao ya ujenzi na uenezi wa chama.

Naye mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Igunga, Mafunda Temanywa, amewataka viongozi hao kuzitunza pikipiki hizo ili ziweze kuleta tija iliyokusudiwa.

“Chama kimewapa pikipiki, na leo mnafundishwa sheria za usalama barabarani, zitumieni pikipiki hizo kwa umakini na kufuata sheria za usalama barabarani ili tija iliyokusudiwa ya kuendelea kukijenga chama chetu CCM itimie,“ amesema Mafunda.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Katibu kata wa CCM kata ya Mwamashimba, Jonas Mondi, alimshukuru mbunge huyo kwa kuwaandalia mafunzo hayo ya usalama barabarani na kuahidi kuwa watazifuata sheria zote walizofundishwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mpina amng’ang’ania Bashe, kumburuza mahakamani pamoja na bodi ya sukari

Spread the loveMbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amesema amenuia kumpeleka mahakamani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Majahazi yadakwa na madumu 1,731 ya mafuta ya kupikia

Spread the loveKikosi kazi cha Polisi Wanamaji Dar es Salaam kimekamata majahazi...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa wa mauaji ya mtoto mwenye ualbino wafikishwa mahakamani

Spread the loveWATUHUMIWA wa mauaji ya Asimwe Novath, mtoto mwenye ualbino, wamefikishwa...

Habari Mchanganyiko

Sangoma awaponza vijeba, watupwa jela maisha kwa kubaka wanafunzi

Spread the loveMAHAKAMA ya wilaya Nkasi Mkoani Rukwa, imemhukumu kifungo cha maisha...

error: Content is protected !!