Sunday , 30 June 2024
Home Habari Mchanganyiko RC Chalamila: Nimeacha ubabe
Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

RC Chalamila: Nimeacha ubabe

Albert Chalamila
Spread the love

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chamalila amemthibishia Rais Samia Suluhu Hassan kuwa sasa ameacha ubabe na kuwataka viongozi wengine wa umma kuacha masuala ya ubabe. Anaripoti Faki Ubwa …(endelea).

Chalamila amebainisha hayo leo Jumanne jijini Dar es Salaam wakati akitoa salamu za mkoa mbele Rais Samia Suluhu Hassan kwenye Kongamano la Maendeleo ya Sekta ya Habari.

“Tuendelee kuwa viongozi wazuri tutakaoepukana na masuala ya kibabe. Wakuu wa Wilaya waliokuwepo hapa simameni Rais awaone Bomboko wa Ubongo na Saad Mtambule wa Kinondoni. Mheshimiwa Rais Meseji yako tumeisikia ingawa mimi nimeshaacha,” amesema Chalamila.

Kauli hiyo ya Chalamila imekuja siku chache baada ya Rais Samia kukemea tena ubabe wa wakuu wa mikoa na wilaya kutokana na kutumia vibaya mamlaka yao ya kumuweka mtu mahabusu kwa saa 48.

Rais Samia alitoa kauli hiyo tarehe 15 Juni mwaka huu wakati akipokea Ripoti ya Kamati ya Utekelezaji wa Mapendekezo ya Tume ya Haki Jinai.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Mpina amng’ang’ania Bashe, kumburuza mahakamani pamoja na bodi ya sukari

Spread the loveMbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amesema amenuia kumpeleka mahakamani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Majahazi yadakwa na madumu 1,731 ya mafuta ya kupikia

Spread the loveKikosi kazi cha Polisi Wanamaji Dar es Salaam kimekamata majahazi...

Habari za SiasaKimataifa

30 wafariki dunia maandamano Kenya

Spread the loveShirika la Human Rights Watch limesema takriban watu 30 walifariki...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa wa mauaji ya mtoto mwenye ualbino wafikishwa mahakamani

Spread the loveWATUHUMIWA wa mauaji ya Asimwe Novath, mtoto mwenye ualbino, wamefikishwa...

error: Content is protected !!