October 17, 2024

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Gachagua akimbilia mahakamani kuzuia kufukuzwa

 

NAIBU Rais wa Kenya Rigathi Gachagua ambaye anakabiliwa na tuhuma mbalimbali, ikiwemo ukosefu wa nidhamu na kumhujumu mkuu wake Rais William Ruto amekimbília mahakani

Vyombo vya habari nchini Kenya vimeripoti kwamba Gachagua siku ya amewasilisha ombi katika mahakama mjini Nairobi akitaka kusitishwa mchakato wa kumuondoa katika nafasi yake ulioanzishwa dhidi yake na wabunge mapema wiki hii.

Washirika wa Rais Ruto waliwasilisha maombi ya kuondolewa kwa Gachagua siku ya Jumanne wakimshtumu kuchochea chuki za kikabila na kudhoofisha serikali.

About The Author