Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Afrika mashariki kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta Tanga

 

RAIS wa Kenya, William Ruto amesema nchi za Afrika Mashariki zinajadili mpango wa kujenga kiwanda cha pamoja cha kusafisha mafuta katika bandari ya Tanga, kikifanana na kile cha Aliko Dangote cha nchini Nigeria.Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam ….(endelea).

Ruto amebainisha kuwa kiwanda hicho kitahudumia nchi kadhaa kwa kutumia mafuta ghafi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Kenya, Sudan Kusini na Uganda.

Kwa upande wake Dangote amesema yuko tayari kujenga kiwanda kama chake chenye uwezo wa kuchakata mapipa 650,000 kwa siku, ikiwa serikali za nchi hizo zitatoa ushirikiano.

About The Author

error: Content is protected !!