MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi imemhukumu Sweetbert Lyankuba (41) mkazi wa Mamba kutumikia kifungo cha miaka 20 jela baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na nyara za serikali nyama ya mnyamapori Nguruwe kiasi cha kilogramu 420. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam ….(endelea).

Hukumu hiyo imetolewa 16 April 2026 na hakimu wa mahakama hiyo Andrew Njau ambapo amesema mtuhumiwa huyo alikuwa akikabiliwa na shitaka la kupatikana na nyara za serikali ambazo alikamatwa nazo akiwa amebeba kwenye baiskeli huko eneo la Kiwanjani katika Hifadhi ya Taifa Katavi.

Njau amesema mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha sheria ya uhifadhi wa wanyamapori kifungu namba 86 (1) (2) (c) (3) ikisomwa pamoja na sheria ya makosa ya uhujumu uchumi kifungu namba 57 (1) 61 (2).

Akisoma hukumu hiyo Njau alisema mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo 23 Oktoba 2025 na kufikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza 14 Novemba 2025, ambapo ameongeza kuwa mahakama imejiridhisha na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo bila shaka na mtuhumiwa kutiwa hatia kwa kosa hilo.

Mshtakiwa huyo licha ya kuomba mahakama hiyo imuonee huruma na kumpunguzia adhabu, mahakama ilitupilia mbali ombi lake na kusema imetoa hukumu hiyo kwa mujibu wa sheria ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!