JESHI la Mapinduzi ya Iran (Islamic Revolutionary Guard Corps) limetangaza kuufunga tena Mlango wa Hormuz, likidai hatua hiyo ni majibu dhidi ya kile walichokiita ‘uharamia’ wa Marekani.Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam ….(endelea).

Uamuzi huo unakuja chini ya saa 24 tangu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, atangaze kuwa njia hiyo imefunguliwa kufuatia makubaliano ya kusitisha mapigano nchini Lebanon.

Kufungwa upya kwa mlango huo muhimu wa usafirishaji wa mafuta kumezua hofu mpya katika masoko ya kimataifa, hasa kutokana na umuhimu wake katika kupitisha sehemu kubwa ya nishati ya dunia.

Mvutano katika eneo hilo umeongezeka tangu mashambulizi ya Marekani na Israel dhidi ya Iran mwishoni mwa Februari, huku wachambuzi wakisema hatua hiyo inaonesha hali ya kutokuwa na uhakika inayoendelea katika ukanda wa Mashariki ya Kati.

About The Author

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

error: Content is protected !!