May 29, 2025

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Mafanikio Makubwa ya Mkutano wa 37 wa ISGE na Kongamano la 28 la AGOTA

 

SHIRIKA la Kimataifa la Endoscopy ya Wanawake (ISGE) na Chama cha Wanaginekolojia na Wakunga wa Tanzania (AGOTA) hivi karibuni walishirikiana kuandaa Mkutano wa 37 wa ISGE pamoja na Kongamano la 28 la AGOTA kuanzia tarehe 21 hadi 24 Mei, 2025, huko Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Tukio hili muhimu lilijumwuisha takriban wajumbe 250 kutoka kote ulimwenguni, na kuunda jukwaa lenye nguvu katika mawanda ya endoscopy na upasuaji wa wanawake kwa njia ya kitobo (MIGS).

Moja ya matokeo makuu ya kongamano ilikuwa ni kutilia mkazo na kujenga uwezo katika eneo hilo. Serikali ya Zanzibar ilionyesha dhamira yake ya kuendeleza afya ya wanawake kwa kusaidia mafunzo ya watoa huduma watano katika endoscopy. Aidha, kuanzishwa kwa Kituo cha Ubora wa Upasuaji wa Laparoscopic katika Hospitali ya Lumumba kunaashiria mkakati unaolingana na vipaumbele vya kitaifa na kimataifa katika afya ya uzazi na mama. Mpango huu unaonyesha umuhimu wa kuwekeza katika huduma za afya kwa wanawake na watoto wachanga hapa nchini.

Kongamano pia lilijumuisha warsha tano za vitendo kabla ya kongamano, ambazo ziliwapa washiriki ujuzi na maarifa kwa vitendo. Warsha zilihusisha mada mbalimbali muhimu, ikiwa ni pamoja na Hysteroscopy, Laparoscopic Suturing, na Warsha ya Wauguzi iliyolenga MIGS.

Katika kongamano, Dk. Murete Lukumay kutoka Tanzania alipokea tuzo kwa uwasilishaji wake kuhusu “Umuhimu wa Maabara ya “Simuleringi” katika kuimarisha Ujuzi wa “Laparoscopic Suturing.” Kazi yake ilisisitiza kujenga uwezo wa upasuaji, hasa katika mazingira fukara na kuhamasisha uchunguzi zaidi wa mbinu bora za mafunzo.

Mkutano ulihudhuriwa na Makamo wa Pili wa Rais wa Zanzibar, ambaye alisisitiza msaada wa serikali kwa mipango ya afya ya uzazi na mama. Uwepo wake ulionyesha umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali na vyama vya kitaaluma katika kushughulikia changamoto za afya zinazokabili wanawake na watoto wachanga.

Kongamano lilihitimishwa na mabadiliko muhimu ya uongozi, ambapo Dk. Anneli Linnamägi kutoka Finland alichaguliwa kuwa Rais mpya wa ISGE, wakati Dk. Sunday Dominic alikabidhiwa urais wa AGOTA. Mabadiliko haya ya uongozi yanaashiria dhamira ya kuendelea kukua na ushirikiano ndani ya mashirika yote mawili, kuhakikisha kuwa malengo ya kuboresha huduma za afya ya uzazi yanabaki kuwa kipaumbele.

Mafanikio ya mkutano huu wa kihistoria unahusisha pia juhudi za kipekee za usimamizi wa tukio. Uratibu wao wa kina, ulijenga mazingira mazuri ya kujifunzia na umakini.

Showtime, kampuni bora ya usimamizi wa matukio ya kwanza Zanzibar, ilicheza jukumu muhimu katika utekelezaji wa mafanikio ya kongamano. Utaalamu wao katika kusimamia matukio adhimu ulihakikisha kuwa kila kipengele, kuanzia uchaguzi wa mahali hadi mambo ya kiufundi, kimeendeshwa kwa weledi. Bwana Ibrahim Mitawi, Mkurugenzi Mtendaji wa Showtime, alisema, “Lengo letu ni kuunda uzoefu bora unaozidi matarajio. Tunajivunia kuchangia mafanikio ya kongamano hili muhimu, kuimarisha ushirikiano na uvumbuzi katika afya ya wanawake.” Dhamira hii ya ubora na ushirikiano inaashiria jukumu muhimu la kitaaluma katika uendeshaji wa mikutano ya kimataifa.

Kwa kumalizia, kongamano la ISGE na AGOTA lilivuka matarajio ya jukwaa la mazungumzo ya kisayansi bali lilisisitiza pia umuhimu wa ushirikiano katika kutatua changamoto za afya duniani. Wakati washiriki wanaporejea katika nchi zao, wanarejes wakiwa na maarifa mapya na dhamira chanya ya kuboresha afya ya wanawake, katika jitihada za pamoja za kuendeleza huduma za afya kwa wanawake na watoto nchini Tanzania na kwengineko.

About The Author

error: Content is protected !!