February 13, 2026

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Mahakam Kuu Z’bar yaitupilia mbali Kesi ya majimbo 17 Zanzibar

Mwenyekiti ACT Wazalendo, Othman Masoud Othman

 

MAHAKAMA Kuu ya Zanzibar imetupilia mbali shauri la kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2025 katika majimbo 17 ya Unguja lililofunguliwa na wagombea wa majimbo hayo kupitia Chama cha ACT-Wazalendo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Uamuzi huo umetolewa leo tarehe 13 Februari 2026, na Jaji Salma Ali Hassan ambaye amesema kuwa shauri hilo limekosa miguu ya kisheria kwa sababu viapo vilivyoendana na maombi yao havikuandaliwa na wakili mwenye leseni ya kulisha viapo.

Aidha uamuzi huo unatokana na pingamizi liliwasilishwa mahakamani hapo na mwanasheria mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Baada ya uamuzi huo Mwanasheria Mkuu wa ACT, Omar Said Shaaban, amesema wanafungua maombi upya ikiashiria msimamo wao kwamba mapambano yanaendelea.

About The Author

error: Content is protected !!