TUNDU Lissu, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), leo tarehe 8 Oktoba 2025, ameelea kumuuliza shahidi wa kwanza wa Jamhuri kwenye kesi Na. . 19605/2025 la uhaini linalomkabili mahakamani hapo ambapo amemtaka shahidi huo kutoa tafrisi ya uasi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Fuatilia dodoso la maswali ya Lissu kwa Shahidi huyo wa kwanza wa Jamhuri ASP George Bagyemu – Naibu Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam aliyeanza kutoa ushahidi wake juzi tarehe 6 Oktoba, kama ifuatavyo :-
Lissu: Sasa tuzungumze kuhusiana na uhaini.
Ulisema kwamba nilielekeza uchunguzi wa uhaini kwasababu Lissu alisema atahamasisha uasi?
Bagyemu: Ni kweli kabisa.
Lissu: Sasa kuna mahali kokote umetafsiri neno uasi?
Bagyemu: Kuzuia uchaguzi, vitisho kwa serikali basi sikusema neno moja moja. kwahiyo sikutoa tafsiri ya neno uasi.
Lissu: Je katika hati ya mashtaka ninayoshtakiwa nayo kuna ufafanuzi wa neno tutahamasisha uasi?
Bagyemu: Huo ufafanuzi upo.
Lissu: Sasa tuambie upo wapi, Hapo kwenye hati ya mashitaka, nakusomea hati ya mashitaka ilivyosema Neno uasi limetajwa mara mbili. Je kuna mahali kokote imeandikwa?
Bagyemu: Uasi ilitafsiriwa.
Lissu: Una akili timamu wewe afisa wa polisi?
Bagyemu: Nina akili timamu ndio maana ni afisa wa Polisi.
Lissu: unaweza kuwa afisa wa polisi nchi hii na ukawa huna akili timamu.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI Digital
ZINAZOFANANA
Mwanajeshi wa Marekani akamatwa na mabomu Tanzania
Machafuko ya 29 Oktoba: Maaskofu Katoliki wataka wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama wawajibike
Shinikizo la kufanyika uchunguzi wa mauaji ya 29 Oktoba lashika kasi