October 8, 2025

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Update kesi uhaini: Lissu ambana shahidi tafsiri ya neno uasi

 

TUNDU Lissu, Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), leo tarehe 8 Oktoba 2025, ameelea kumuuliza shahidi wa kwanza wa Jamhuri kwenye kesi Na. . 19605/2025 la uhaini linalomkabili mahakamani hapo ambapo amemtaka shahidi huo kutoa tafrisi ya uasi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Fuatilia dodoso la maswali ya Lissu kwa Shahidi huyo wa kwanza wa Jamhuri ASP George Bagyemu – Naibu Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam aliyeanza kutoa ushahidi wake juzi tarehe 6 Oktoba, kama ifuatavyo :-

Lissu: Sasa tuzungumze kuhusiana na uhaini.

Ulisema kwamba nilielekeza uchunguzi wa uhaini kwasababu Lissu alisema atahamasisha uasi?

Bagyemu: Ni kweli kabisa.

Lissu: Sasa kuna mahali kokote umetafsiri neno uasi?

Bagyemu: Kuzuia uchaguzi, vitisho kwa serikali basi sikusema neno moja moja. kwahiyo sikutoa tafsiri ya neno uasi.

Lissu: Je katika hati ya mashtaka ninayoshtakiwa nayo kuna ufafanuzi wa neno tutahamasisha uasi?

Bagyemu: Huo ufafanuzi upo.

Lissu: Sasa tuambie upo wapi, Hapo kwenye hati ya mashitaka, nakusomea hati ya mashitaka ilivyosema Neno uasi limetajwa mara mbili. Je kuna mahali kokote imeandikwa?

Bagyemu: Uasi ilitafsiriwa.

Lissu: Una akili timamu wewe afisa wa polisi?

Bagyemu: Nina akili timamu ndio maana ni afisa wa Polisi.

Lissu: unaweza kuwa afisa wa polisi nchi hii na ukawa huna akili timamu.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI Digital

About The Author

error: Content is protected !!