Ndege ya Cristiano Ronlado
NDEGE binafsi ya mchezaji nyota wa soka wa kimataifa, Cristiano Ronaldo, imeondoka ghafla nchini Saudia Arabia. Anaripoti Joyce Ndeki, Dar es Salaam … (endelea).
Taarifa zinasema, ndege ya Ronaldo, imeondoka Riyadhi usiku wa kuamkia leo, kuelekea Madrid, nchini. Hispania.
Kuondoka kwa ndege hiyo kutoka Riyadh kuelekea Madrid, kumefungua mjadala mpana kuhusu hali ya usalama nchini Saudi Arabia, wakati huu ambako mvutano wa kijeshi ukiendelea kuongezeka eneo la Mashariki ya Kati.
Mvutano huo, unatokana na hatua ya Marekani na mshirika wake mkuu Israel, kuishambulia kijeshi Iran, ambayo nayo inalipiza kisasi kwa kushambulia maslahi ya Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati.
Taarifa zinasema, Riyadh imekumbwa na mashambulizi ya anga yanayohusishwa na mvutano huo kati ya Marekani na Iran.
Pamoja na kutokuwapo tamko rasmi linalothibitisha kuwa Ronaldo ameondoka nchini humo kwa sababu za kiusalama, lakini kuondoka kwa ndege yake, kunaonyesha mwanasoka huyo hayuko tena Riyadhi.
Ronaldo anaishi Riyadh na familia yake tangu alipojiunga na klabu ya Al-Nassr FC, na kwamba amekuwa sura muhimu ya kampeni ya Saudi Arabia kujitangaza kama kitovu kipya cha michezo ulimwenguni.
Kuondoka kwa mwanamichezo huyo, hata kwa muda, kunaweza kutafsiriwa kama ishara ya tahadhari katika kipindi hiki cha sintofahamu ya kijeshi.
Kwa mujibu wa data za ufuatiliaji wa safari za anga, ndege aina ya Bombardier Global – Express 6500, iliondoka Riyadh majira ya saa 8:00 usiku, ikapitia anga ya Misri na Bahari ya Mediterania kabla ya kutua Madrid saa 1:00 asubuhi.
ZINAZOFANANA
Nani alifariki pamoja na Ali Khamenei?
Mahakama yaamuru Wakazi kumlipa Mil 100 Baba Levo
Rais wa FA ya Congo afungwa maisha jela