Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Walid Alhad Omari
VIONGOZI wa madhehebu ya kidini nchini, wamefanya matembezi ya amani leo Jumamosi, tarehe 20 Septemba, jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
“Viongozi wa dini zote, wanafanya matembezi ya amani na sio kufanya uchawa. Ni kuliombea taifa amani, ili izidi kudumu kwenye taifa hili,” ameelza Sheikh wa mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Walid Alhad Omari.
Matembezi hayo yameanzia viwanja vya Mnazi Mmoja hadi viwanja vya mashujaa, kuelekea siku ya Amani Duniani ya 21 Septemba ya kila mwaka.
Hata hivyo, kiongozi huyo hakuzungumzia suala la haki, linalotajwa na wachambuzi wa masuala ya demokrasia, kuwa ndio msingi mkuu wa taifa kuwa na amani.
ZINAZOFANANA
Mwanajeshi wa Marekani akamatwa na mabomu Tanzania
Machafuko ya 29 Oktoba: Maaskofu Katoliki wataka wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama wawajibike
Shinikizo la kufanyika uchunguzi wa mauaji ya 29 Oktoba lashika kasi