LEO tarehe 23 Juni 2025, Mwenyekiti wa Ngome ya Wanawake wa Chama cha ACT-Wazalendo, Janeth Rithe amepewa dhamana. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea). Rithe aliyekuwa anashikiliwa na Polisi katika Kituo cha Polisi cha Kati ameachiwa kwa sharti kwamba aripoti tena Polisi siku ya Jumatano tarehe 25 Juni 2025. Rithe aliyejisalimisha mikononi mwa Jeshi hilo tarehe 20 Juni 2025, na kuhojiwa. Si jeshi la Polisi au ACT waliosema Rithe alihojiwa kwa kosa gani. Tarehe 18 Juni 2025, akiwa viwanja vya Bakharesa-Manzese jijini Dar es Salaam, kwenye mkutano wa hadhara wa chama hicho alionesha kushangazwa na kauli ya Rais Samia kuhusu hali ya uchumi wa Marekani. Share this… Facebook Pinterest Twitter Linkedin Whatsapp About The Author Erasto Masalu See author's posts Post navigation ACT Wazalendo: Deni la Taifa linakuwa kwa kasi, uchumi wa nchi hatarini Iran yashambulia kambi za Marekani Qatar, Iraq