MBUNGE wa Jimbo la Kigambo (CCM) na Mkurugenzi mteule wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Kanda ya Afrika, Faustine Ndungulile amefariki Dunia usiku wa kuamkia leo tarehe 27 Novemba 2024, nchini India alipokuwa akipatiwa matibabu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam ,,, (endelea). Taarifa ua kifo chake imethibitishwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Akson. “Nimepokea kwa masikito makubwa taarifa ya kifo cha Mbunge wa Kigamboni na Mkurugenzi mteule wa Shirika la Afya Dunia (WHO), kanda ya Afrika Mheshimiwa Dk. Faustine Ndungulile” “Kwa niaba ya Bunge natoa pole kwa Familia, wakazi wa Kigamboni na Watanzania wote.” Alisema Dk Tulia Aidha katika taarifa yake imeeleza kuwa, Ofisi ya Bunge kwa Kushirikiana na Familia inaendelea kuratibu shughuli za mazishi na taarifa zaidi zitatolewa. Dk Ndungulile amefariki Dunia ikiwa zimepita siku 90 Toka alipoteuliwa kuwa mkurugenzi wa (WHO) kwa Kanda ya Afrika tarehe 27 Agosti 2024. Share this… Facebook Pinterest Twitter Linkedin Whatsapp About The Author Erasto Masalu See author's posts Post navigation Ushiriki wa Rais Samia G20 wainufaisha Tanzania Sakata la mgombea Chadema aliyeuwa kwa risasi, Polisi yamshikilia askari Magereza
Kuchaguliwa Bwana, Kuchaguliwa Huko Vijiji 97, Mitaa 36, Tongoji 853, WajumbeH 1,222, WajumbeM 101 = 2,309 Jenga Nyumba ya Tembe Tuuu hapo gharama nguvu zako na Jasho na kaharufu ka mwili kidogo Ndio maana tuwape hongera wananchi kwa kuwa.. Chadema ikishinda (Kimyaaaa mtaa wote kichekooo) Chadema ikishindwa (Tumeibiwa kura – Hakuna uchaguzi kuna uchafuzi – Kura feki – Polisi wamewasaidia) Inahitaji JESHI, Polisi, FBI (Kwa sababu ya watalii wanaokuja Zanzibar na Kilimanjaro – Watalii hawawezi kuja Tanzania kuangalia viazi utamu au machungwa ya Tanga), ICC, kujua aina ya Siasa zinazofanyika Tanzania Hata malengo ya maendeleo endelevu wamekupiga bao la kisigino sema tu hawatakiwi kutangazwa Reply