
WAZIRI wa mambo ya nje wa Israel amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) António Guterres ”Hana ruhusa” kuingia Israel na amepigwa marufuku nchini humo.
Israel Katz anasema uamuzi wake unafuatia hatua ya Guterres “kutolaani” shambulio la kombora la Iran dhidi ya Israel siku ya Jumanne.
Anamshutumu mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa kwa kuwa “mpinzani wa Israel” na kutoa “msaada kwa magaidi, wabakaji na wauaji.Guterres atakumbukwa kama doa katika historia ya Umoja wa Mataifa kwa vizazi vijavyo.”
Jana, mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa alilaani “kuongezeka kwa mzozo wa Mashariki ya Kati” na kutoa wito wa kusitishwa kwa mapigano.
ZINAZOFANANA
Vita vya Gaza: Hamas waapa kufia kwenye ardhi yao
Maadhimisho ya Nne ya Lugha ya Kiswahili yapokewa kwa bashasha Harare, Zimbabwe
Diogo Jota wa Liverpool afariki kwa ajalin