WATU 11 wamepoteza maisha na wengine 44 wamejeruhiwa baada ya basi la Kampuni ya A-N Coach lenye namba ya usajili T282 CXT kupata ajali katika eneo la Luanjilo Wilaya ya Mbeya Vijijini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea).
Ajali hiyo imetokea alfajiri ya leo Ijumaa, Septemba 6, 2024 baada ya basi hilo lililokuwa likitoka Mbeya kwenda Tabora kupinduka wakati likilikwepa lori, kisha kutumbukia mtaroni.
Mganga wa Mkuu wa Hosptali ya Wilaya ya Chunya, Dk. Darson Andrew amethibitisha kupokea idadi ya hiyo na vifo huku akieleza kati ya majeruhi 44 wanne wana hali mbaya na watapewa rufaa kupelekwa Hosptali ya Rufaa Kanda ya Mbeya.
ZINAZOFANANA
Kesi ya uhaini ya Lissu kusikilizwa siku 26 mfululizo
Mvutano wa kisheria wagubika Mahkama ya Z’bar
Singida waipa kongole RITA kutoa vyeti vya kuzaliwa ndani ya saa 48