WATU 11 wamepoteza maisha na wengine 44 wamejeruhiwa baada ya basi la Kampuni ya A-N Coach lenye namba ya usajili T282 CXT kupata ajali katika eneo la Luanjilo Wilaya ya Mbeya Vijijini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya … (endelea).
Ajali hiyo imetokea alfajiri ya leo Ijumaa, Septemba 6, 2024 baada ya basi hilo lililokuwa likitoka Mbeya kwenda Tabora kupinduka wakati likilikwepa lori, kisha kutumbukia mtaroni.
Mganga wa Mkuu wa Hosptali ya Wilaya ya Chunya, Dk. Darson Andrew amethibitisha kupokea idadi ya hiyo na vifo huku akieleza kati ya majeruhi 44 wanne wana hali mbaya na watapewa rufaa kupelekwa Hosptali ya Rufaa Kanda ya Mbeya.
ZINAZOFANANA
Machafuko ya 29 Oktoba: Maaskofu Katoliki wataka wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama wawajibike
Shinikizo la kufanyika uchunguzi wa mauaji ya 29 Oktoba lashika kasi
Meridianbet yaendelea kuwekeza kwa jamii kupitia MRC Rehabilitation Centre