
TAARIFA iliyotolewa na Hamas imesema kuwa Haniyeh ameuawa katika shambulio lililofanywa na Wazayuni (Israel) mjini Tehran, Iran. Inaripiti Mitandao ya Kimaraifa.
Katika taarifa yake Jumatano asubuhi, Hamas ilisema Haniyeh aliuawa katika uvamizi wa Israel alipokuwa ziarani Tehran kuhudhuria kuapishwa kwa Rais Masoud Pezeshkian.
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Iran pia limethibitisha kifo chake
Wanajeshi wa Israel na viongozi wakuu ndani ya serikali yake bado hawajajibu madai hayo.
ZINAZOFANANA
ACT Wazalendo: Deni la Taifa linakuwa kwa kasi, uchumi wa nchi hatarini
ACT Wazalendo hawajui hatma ya Janeth Rithe
Maftaha ajiunga ACT pamoja na wanachama 2,567 wa CUF