
Marco Kilo
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimelaani kitendo cha Mwandishi wa Televisheni ya EATV, Marco Kilo kushambuliwa na maofisa wa Kampuni ya mabasi ya mwendokasi (UDART). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Tarifa ya Brenda Rupia, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa chama hicho ya leo tarehe 6 Septemba 2025, imesema kuwa chama hicho kinatoa wito kwa jeshi la Polisi kuchukua hatua ya haraka za kisheria dhidi ya maofisa UDART waliohusika kumsambulia Kilo, tarehe 4 Septemba 2025.
“Chadema tunatoa wito kwa Jeshi kwa Jeshi la Polisi kuchukua hatua za haraka za kisheria dhidi ya maofisa wa UDART waliohusika katika tukio hilo,” imeeleza taarifa ya Rupia.
Rupia ametoa wito kwa vyombo vya habari, taasisi za haki za binadamu kuhakikisha mwandishi Kilo anapata haki yake.
ZINAZOFANANA
Askofu Mwanamapinduzi akimbia nchini akidai kusakwa kuuwawa
TMA yatangaza kupatwa kwa mwezi Sept 7
Bosi wa JamiiForum ajiuzulu ujumbe wa Tume ya Ulinzi ya Taarifa Binafsi