RAIS wa Comoro, Azali Assoumani amejeruhiwa katika shambulio la kisu, mamlaka zimesema.
“Asante Mungu, maisha yake hayako hatarini,” amesema msemaji wa serikali. MORONI, Comoro
Alidungwa kisu alipokuwa akihudhuria mazishi ya kiongozi wa kidini karibu na mji mkuu Moroni lakini “alijeruhiwa kidogo” na amerejea nyumbani, msemaji Fatima Ahamada aliambia shirika la habari la Reuters.
Aliongeza kuwa mshambuliaji alikamatwa.
ZINAZOFANANA
Bunge laanzisha mchakato kumwondoa Rais Macron
Milio ya risasi yasikika katika mji mkuu wa Mali
Baa la njaa laikumba Sudan