Azali Assoumani
RAIS wa Comoro, Azali Assoumani amejeruhiwa katika shambulio la kisu, mamlaka zimesema.
“Asante Mungu, maisha yake hayako hatarini,” amesema msemaji wa serikali. MORONI, Comoro
Alidungwa kisu alipokuwa akihudhuria mazishi ya kiongozi wa kidini karibu na mji mkuu Moroni lakini “alijeruhiwa kidogo” na amerejea nyumbani, msemaji Fatima Ahamada aliambia shirika la habari la Reuters.
Aliongeza kuwa mshambuliaji alikamatwa.
ZINAZOFANANA
Iran yathibitisha kuwa Waziri wa Ujasusi ameuawa
Mojtaba Khamenei yuko salama kiafya na anaongoza kikamilifu – Iran
Iran yaapa kumuua Benjamin Netanyahu