Thom Lukuvi
WILLIAM Lukuvi, aliyekuwa mbunge wa jimbo la Isimani na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), atakumbukwa kama nguzo muhimu aliyekuwa akishikilia mshikamano wa familia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Mwanasiasa huyo anayetarajiwa kupumnzishwa kijijini kwao Idodi Iringa vijijini 31 Machi, alifariki dunia Jumatano iliyopita, mkoani Dodoma.
Akizungumza nyumbani kwao mtoto wa kaka yake na marehemu Lukuvi Thom Lukuvi anaeleza kuwa marehemu hakuwa tu kiongozi wa kisiasa, bali pia mlezi na mshauri aliyekuwa tayari kusimama na mtu yeyote aliyehitaji msaada.
Amesema katika maisha yake ya kila siku, William Lukuvi alijulikana kwa moyo wake wa kusaidia wengine somo ambalo amewaachia kwa wanafamilia
Thom amesema kuwa Familia inaeleza kuwa misingi ya haki na ukweli ndiyo iliyomuongoza katika maamuzi yake yote kwani alisimamia usawa, na haki, bila upendeleo sifa ambazo zilimtofautisha na kumfanya kuwa mfano wa kuigwa, si tu kwa familia yake bali pia kwa jamii nzima.
ZINAZOFANANA
Wazili Mkuu kuongoza mazishi ya Kitaifa ya Lukuvi Idodi Iringa
Meridianbet yaweka alama muhimu kwa kuwakumbuka wagonjwa waliolazwa
NBC yahitimisha Kampeni Kuhamasisha Kilimo cha Korosho Tandahimba, yakabidhi trekta kwa TANECU