December 13, 2025

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Rais Samia aongoza waombolezaji ibada ya mazishi ya Jenesta

 

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewaongoza waombolezaji kushiriki ibada ya mazishi ya mbunge wa Peramiho (CCM) Jenista Mhagama. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Ibada hiyo inafanyika hii leo tarehe 13 Desemba 2025 kwenye Parokia ya Mwenyeheri Maria Theresa kiwanja cha Ndege, jijini Dodoma.

Jenista ambaye alifariki tarehe 11 Desemba 2025, mwili wake utaagwa hii leo jijini humo na kisha kusafirishwa mpaka Peramiho mkoani Ruvuma ambapo mazishi yatafanyika Jumanne ya tarehe 16 Desemba 2025 kijiji cha Ruanda, Mbinga mkoani Ruvuma.

Mpaka umauti unamkuta Jenista alikuwa Mbunge wa jimbo la Peramiho ambalo amehudumu kwa miaka 20.

About The Author

error: Content is protected !!