
Afisa Takukuru mkoani Iringa, Ditram Muhoma
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), mkoani Iringa, imeweka msimamo mkali dhidi ya wagombea wanaojihusisha na kutoa ahadi za uongo wakati huu wa kampeni. Anaripoti Zakia Nanga, Iringa … (endelea).
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Iringa, Afisa Takukuru mkoani Iringa, Ditram Muhoma amesema, wagombea wote wa ubunge na udiwani, wanatakiwa kuzingatia kikamilifu ahadi zilizoainishwa kwenye Ilani rasmi za vyama vyao, badala ya kutumia maneno matamu au matarajio yasiyotekelezeka kama chombo cha kuwashawishi wapiga kura.
Amesema, tabia hiyo si tu ya kupotosha umma, bali ni aina ya rushwa ya kisiasa inayodhoofisha misingi ya demokrasia na uwajibikaji.
Kwa mujibu wa afisa huyo, Takukuru inafuatilia kauli za wagombea wote wa ubunge na udiwani mkoani Iringa. Amesema, wale ambao hawatazingatia Ilani zao na hivyo, kutoa ahadi kinyume na maelezo hayo, watachukuliwa hatua za kisheria.
Hata hivyo, afisa huyo, hakutaja wagombea ambao tayari wameanza kukiuka taratibu hizo.
ZINAZOFANANA
Mpina ashinda kesi, mahakama yamruhusu kurudisha fomu
TMA yatangaza utabiri wa mvua za vuli za Oktoba mpaka Desemba
Mahakama kuamua hatma ya Lissu Jumatatu