RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Wawakilishi, Dk Hussein Mwinyi, amewataka viongozi wa dini, wanasiasa, waandishi wa habari na wananchi kukemea kauli zinazoweza kuvuruga amani katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).
Ametoa kauli hiyo leo, tarehe 5 Septemba, 2025 alipokuwa akizungumza kwenye Baraza la Maulid, lililofanyika Zamzibar na kusema hakuna taifa linaloweza kudumu bila amani na kuwataka wanasiasa kuepuka siasa za chuki na mifarakano.
Aidha amewahimiza waumini wa kiislamu kufuata mafunzo ya dini yao ili kudumisha mshikamano huku pia akisisitiza kuwa Amani na utulivu ni tunu.
ZINAZOFANANA
Dk. Homera azitaka bodi za Udhamini kujiepusha na ubadhirifu wa mali za umma
Mahakama yaamuru kujengwa kizimba maalumu kwa ajili ya mashahidi wa siri
DED Yegella: Fedha za ndani kunufaisha kata zote Mbeya DC