HATIMAYE Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Victoria, Ezekiel Wenje, amejitokeza hadharani na kupinga uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba 2025. Anaripoti Zakia Nanga, Dar es Salaam … (endelea).
Wenje amekuwa kimya tangu aliposhindwa na John Heche kwenye kinyang’anyiro cha kuwania umakamu mwenyekiti wa Chadema katika uchaguzi uliofanyika tarehe 22 Januari 2025, amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeshindwa kuwasikiliza wananchi.
“CCM watalipa gharama, sisi tuendelee kupigania mabadiliko, wafuasi wa Chadema na wananchi tuendeleze mapambano ya kudai mabadiliko ya kisiasa na kikatiba nchini”
Chadema kimekataa kushiriki uchaguzi wa mwaka huu hadi mabadiliko ya sheria na mifumo ya uchaguzi ifanyike.
ZINAZOFANANA
Ronaldo akimbia vita Saudia, aelekea Madrid
Vigogo hawa wameondoka, katika vita kati ya Marekani na Iran
Ayatollah Ali Khamenei: Kiongozi Mkuu wa Iran athibitika kuawa