
SERIKALI imesema kuwa inatarajia kukusanya kiasi cha Sh. 56.49 trilioni kwa ajili ya bajeti ya mwaka 2025/2026. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Akiwasilisha Bajeti hiyo Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha, amesema kuwa sura ya Bajeti inaonesha kuwa jumla ya Sh. 56.49 trilioni zinatarajiwa kukusanywa na kutumika katika mwaka 2025/26.
“Bajeti hii inatarajiwa kugharamiwa na mapato ya ndani ya sh. 40.47 trilioni, misaada sh.1.07 trilioni, na mikopo ya sh.14.95 trilioni, Kati ya mapato ya ndani yanayotarajiwa, mapato ya kodi ni sh. 32.31 trilioni, mapato yasiyo ya kodi sh. 6.48 trilioni na mapato ya Mamlaka za Serikali za Mitaa Sh.1.68 trilioni.
Aidha, mikopo inajumuisha Sh. 6.27 trilioni, kutoka vyanzo vya ndani na Sh. 8.68 trilioni kutoka vyanzo vya nje,” amesema Wazari Mwigulu.
ZINAZOFANANA
Mpina ashinda kesi, mahakama yamruhusu kurudisha fomu
TMA yatangaza utabiri wa mvua za vuli za Oktoba mpaka Desemba
Takukuru yaonya wagombea wanaolipuka na ahadi za kampeni