HATIMAYE yametimia, Gazeti la MwanaHALISI toleo Na.507 la tarehe 8 -14 Mei 2025 lilifichua kuwa kundi la G55 litajiunga na Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMA) hatimaye leo tarehe 19 Mei kundi hilo limejiunga na chama hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Mwenyekiti wa chama hicho Hashimu Rungwe amewapokea wanasiasa hao waliovuna vyeo katika chama hicho.
Kamati Kuu ya Chama hicho ilizijaza nafasi zilizokuwa wazi katika chama hicho ambazo ni pamoja na Katibu Mkuu ambayo ameteuliwa Salum Mwalimu, Devotha Minja akikaimu nafasi ya Makamu Mwenyekiti Bara na Benson Kigaila akikaimu nafasi ya Naibu katibu Mkuu Bara.
ZINAZOFANANA
Dk. Homera azitaka bodi za Udhamini kujiepusha na ubadhirifu wa mali za umma
Mahakama yaamuru kujengwa kizimba maalumu kwa ajili ya mashahidi wa siri
DED Yegella: Fedha za ndani kunufaisha kata zote Mbeya DC