
Ian Khama
RAIS wa zamani wa Botswana, Ian Khama amerejea nchini bila kutarajiwa baada ya miaka mitatu ya kukaa uhamishoni, na kufikishwa mahakamani kujibu mashtaka yakiwemo ya kutakatisha fedha na kumiliki silaha kinyume cha sheria. GABORONE, Botswana.
Mzee huyo mwenye umri wa miaka 71 alikuwa amedai hivi majuzi kulikuwa na njama ya kumtilia sumu ikiwa angekanyaga nyumbani kwake.
Serikali ilizitaja tuhuma hizo kuwa za “kuudhi”.
Wafuasi wake waliimba “Jenerali amerejea” wakati Khama akiondoka kwenye mahakama siku ya Ijumaa katika mji mkuu, Gaborone
ZINAZOFANANA
Trump: Uchumi wa Marekani upo katika kipindi cha mpito
Papa Francis atoa kauli yake ya kwanza, awashukuru wanaomuombea
Korea Kusini kuchangia USD Mil 104 maboresho ya Muhimbili