September 19, 2024

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Polisi: Hatujapiga marufuku mikutano ya hadhara

Msemaji wa Polisi, DCP David Misime

 

JESHI la Polisi limesema halijapiga marufuku kufanyika mikutano ya nje ya hadhara na ile ya ndani ili mradi inafuata matakwa ya sheria za nchi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 12 Agosti 2024 na Msemaji wa Jeshi hilo nchini, DCP – David Misime, killichopigwa marufuku ni mkusanyiko uliokuwa umeitishwa na Viongozi wa Chadema huko Jijini Mbeya kwa kivuli cha kuadhimisha Siku ya Vijana Duniani.

Hayo yanajiri wakati Baraza la Vijana Chadema (BAVICHA) likiwa limeratibu kongamano la maadhimisho ya siku ya vijana duniani lililotarajiwa kufanyika katika viwanja vya Ruanda Nzovwe jijini Mbeya.

Maadhimisho hayo ambayo yalikuwa yafanyike leo Jumatatu, mgeni rasmi alitarajiwa kuwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.

About The Author