March 15, 2026

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Mojtaba Khamenei yuko salama kiafya na anaongoza kikamilifu – Iran

Mojtaba Khamenei

 

WAZIRI wa masuala ya kigeni wa Iran, Abbas Araghchi, amesema Alaraby Aljadeed kwamba Mojtaba Khamenei yuko salama na mwenye afya njema” na “anaongoza kikamilifu.”

Mojtaba (56), hajajitokeza hadharani tangu alipoteuliwa kuongoza taifa hilo, tarehe 8 Machi mwaka huu, kufuatia kifo cha Ayatollah Ali Khamenei, aliyeuawa katika mashambulizi ya Marekani na Israeli.

Hotuba yake ya kwanza kwa umma ilirushwa na vyombo vya habari vya serikali mnamo 12 Machi, ikasomwa na mtangazaji.

Mojtaba Khamenei ameteuliwa kuwa kiongozi mkuu mpya wa Iran na mrithi wa baba yake, Ayatollah Ali Khamenei, ambaye aliuawa siku ya kwanza ya vita na Marekani na Iran.

Baadhi ya umati wa watu wanaounga mkono uanzishwaji wa jeshi wamejitokeza mitaani kusherehekea uteuzi wa mtu mwenye msimamo mkali karibu na Kikosi chenye nguvu cha Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC).

Lakini Wairani wengine wameiambia BBC kwamba wanaamini haitaleta mabadiliko.

“Hata nafasi ndogo kabisa za mabadiliko hazipo tena ndani ya mfumo,” alisema mtu mmoja mwenye umri wa miaka 30 katika mji mkuu, Tehran.

Alisema Baraza la Wataalamu, chombo cha viongozi wa dini chenye wajumbe 88 kinachomchagua kiongozi mkuu, hakingeweza kumchagua mtu yeyote aliye karibu na Ali Khamenei.

“Kwa hivyo, kila kitu kitabaki vile vile; hawahitaji hata kubadilisha nyimbo zao ili kumuunga mkono kiongozi mpya,” aliongeza.

Kwa miaka mingi, kumekuwa na uvumi kwamba Mojtaba Khamenei alikuwa na ushawishi mkubwa nyuma ya pazia nchini Iran.

Mojtaba Khamenei anatajwa kuwa”mkandamizaji zaidi kuliko baba yake,” anaeleza mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 20 huko Tehran.

Anaongeza: “Natumai kweli maisha yao [maafisa wakuu] yataisha katika vita, vinginevyo tukiwa chini ya utawala wake, sote tutakufa.”

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Tehran, Araghchi amesema, Iran haitaki vita na majirani zake kwa kuwa undugu wao, hauwezi kugombanishwa na Marekani.

Hata hivyo, amewataka mataifa jirani, kufukuza aliowaita, “wavamizi kwenye nchi zao.” Alikuwa akilenga kambi za kijeshi za Marekani zilizopo eneo la Mashariki ya Kati.

Araghchi amesema kuwa Iran inakaribisha “mpango wowote wa kikanda ambao utaweza kuleta mwisho wa haki wa vita.”

Amesema, Bahari ya Hormuz “iko wazi kwa kila mtu isipokuwa meli za Marekani na washirika wake.

Aidha, Araghchi amesema kuwa “hakuna mpango maalum ulio mezani hadi sasa wa kumalizia vita.”

About The Author

error: Content is protected !!