Tundu Lissu akiwa mahakamani
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema, Tundu Lissu, leo anaweza kuanza kuandika historia yake nyingine, wakati Mahakama Kuu, itakapotolea maamuzi pingamizi lake dhidi ya serikali. Anaripoti Saed Kubenea, Dar es Salaam … (endelea).
Iwapo pingamizi la Lissu dhidi ya uhalali wa shahidi wa tatu wa serikali, Samwel Kaaya, kuwasilisha vielelezo vyake mahakamani hapo, linatajwa na watalaamu wa sheria kuwa “linabeba kesi mzima.”
Iwapo pingamizi la mwenyekiti litakubaliwa, hakuna shaka kwamba kesi mzima ya serikali, itakosa nguvu,” ameeleza mmoja wa mawakili wa Chadema kwa sharti la kutitajwa gazetini.
Kesi dhidi ya Lissu, inasikilizwa na jopo la majaji watatu linaloongozwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu – Dunstan Ndunguru, James Karayemaha na Ferdinand Kiwonde.
Tayari mashahidi wawili wa Jamhuri wameshakamalisha kutoa ushahidi wao.
ZINAZOFANANA
TRA yawataka wanachama wa SACCOS kuhamasisha ulipaji kodi
Mwanasheria wa kimataifa ataka Tanzania isifukuzwe Jumuiya ya Madola
Mwabukusi amuonya RC Chalamila, amtaja sakata la 29 Oktoba