MAHAKAMA Kuu, Masjala Ndogo ya Dar es Salaam, imemhukumu Suleiman Kwata adhabu ya kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya mauaji ya makusudi dhidi ya Editha Charles, mfanyakazi wa ndani. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Kwa mujibu wa hukumu hiyo, tukio hilo lilitokea tarehe 6 Julai 2022, katika eneo la Kimara Temboni, Wilaya ya Ubungo.
Mahakama imeeleza kuwa mshtakiwa, ambaye alikuwa jirani wa marehemu, alimuua Editha kwa kumchoma kisu shingoni baada ya kushirikiana naye kuvunja kibubu na kuiba fedha za mwajiri wake kiasi cha Sh. 16 milioni.
Imeelezwa kuwa wakati wakiendelea kufanya uhalifu huo, mshtakiwa alidaiwa kuingiwa na tamaa ya ngono na kutaka kumwingilia kimwili Editha. Alipokataa, alimshambulia kwa nguvu na kumbaka.
Tukio hilo lilimkasirisha marehemu, ambaye alimtishia kumfichua kwa mwajiri wake. Hapo ndipo mshtakiwa alipomchoma kisu na kusababisha kifo chake.
ZINAZOFANANA
Mtanzania aliyeuwawa na Hamas arudishwa Tanzania
Rais Samia aunda Tume ya kuchunguza matukio ya 29 Oktoba
Maandamano ya Gen Z kuikosesha Tanzania mabilioni