
KAMPUNI ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na dLab inaendelea kuwawezesha wasichana wenye umri wa miaka 14-18 kwa ujuzi wa STEM kupitia programu ya ‘Code Lie A Girl’. Mpango huu umewawezesha zaidi ya wahitimu 3,000 katika mikoa mbalimbali, ikiwemo Arusha, Dar es Salaam, Mbeya, Dodoma, na Mwanza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Hafla ya mahafali iliyofanyika jijini Dar es Salaam iliongozwa na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Vodacom Tanzania Plc, Vivienne Penessis akizungumza na wanafunzi na kuwakabidhi zawadi wahitimu huku akisisitiza dhamira ya Vodacom ya kuwawezesha wasichana kwa ujuzi wa programu (coding) na uvumbuzi.
Programu hii pia inahimiza ujumuishi kwa ushirikishaji wa wasichana wenye ulemavu, ikionyesha azma ya Vodacom ya kuziba pengo la kijinsia katika teknolojia ya kidijitali.

ZINAZOFANANA
Tata yaja na mpango wa kusafirisha mizigo mikubwa, wakulima watajwa kunufaika
NBC yaitambulisha “NBC Shambani’’ kwa wakulima wa Ufuta Pwani
Meridianbet yazindua “GIFT WEDNESDAY” shinda Samsung A25 mpya kila wiki