February 5, 2025

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Lungu akwama kuwania urais Zambia

Edgar Lungu

 

Mahakama ya Katiba imetoa uamuzi kuwa, rais wa zamani wa Zambia, Edgar Lungu, hawezi kugombea tena urais kwa sababu ameshaongoza vipindi viwili vinavyoruhusiwa kisheria. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Lungu mwenye umri wa miaka 68 kwanza alichaguliwa kuongoza Januari 2015 kumalizia miezi 20 iliyosalia baada ya mtangulizi wake

Michael Sata kufariki dunia Oktoba 2014.

Lungu ambaye amechaguliwa na muungano wa Tonse kuwania urais 2026 aliitoa hoja kwamba kipindi hicho kisifikiriwe kwani hakutumikia kipindi kuzima cha miaka mitano. Lakini mahakama ilipinga hoja hiyo, hivyo ikabatilisha uamuzi wa awali ambao ulimsafishia njia kuwania muhula mwingine miaka mitatu baada ya kuangushwa na Hakainde Hichilema

About The Author

error: Content is protected !!