WAZIRI Mkuu Mwigulu Nchemba leo 5 Januari 2026 amefungua Skuli ya Sekondari Chukwani, Zanzibar ikiwa ni sehemu ya shamrashamra ya maadhimisho ya Miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar. Anaripoti Zakia Nanga, Zanzibar … (endelea).
Ujenzi wa skuli hiyo ambayo imegharimu shilingi bilioni 6.1 imeanzishwa kwa lengo la kuwaandaa vijana wenye maarifa, ujuzi, ubunifu na maadili, kwa kuunganisha nadharia na vitendo na hivyo kuwa na manufaa mengi ikiwemo kuongeza fursa za elimu bora kwa watoto wa Zanzibar.
Mwigulu amempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Hussein Mwinyi kwa uwekezaji mkubwa alioufanya katika sekta ya elimu.
ZINAZOFANANA
Mfumo mpya wa Elimu kuanza rasmi 2028
Shule za sekondari, Veta kufungiwa miundombinu ya nishati safi ya kupikia
Wanafunzi 937,581 wachaguliwa kujiunga kidato cha kwanza, wasichana vinara