WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amekutana na Watumishi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), na kuwakumbusha wajibu wao wa kuunganisha serikali kimtandao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Mkutano na watumishi hao, umefanyika katika ofisi za mamlaka hiyo jijini Dodoma.
Katika ziara hiyo iliyofanyika jana 24 Novemba 2025, Waziri Kikwete aliambatana na viongozi wengine akiwemo Naibu Waziri Ofisi ya Rais Utumishi, Regina Qwaray na Katibu Mkuu Ikulu, Mululi Mahendeka.
Alisema: “Naikumbusha mamlaka kuwa ina wajibu wa kuendelea kuhakikisha inasimamia na kuendeleza kazi ya kuunganisha serikaki kimtandao na kimifumo,” na kuongeza, hiyo itasaidia serikali kuendelea kuwa salama kidigitali.
ZINAZOFANANA
Wanafunzi 77 wafutiwa matokeo ya kidato cha nne, ufaulu wapanda
Uwekezaji wa Samia, wanafunzi 16 wasomea Data Science na AI Afrika Kusini
Meridianbet yawakumbuka wanaopitia maisha magumu Kinondoni