
John Mnyika, Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema
KESI ya mgawanyo wa mali iliyofunguliwa na Said Issa Mohamed, aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Visiwani na wenzake wawili, dhidi ya Bodi ya Wadhamini ya Chadema na katibu mkuu wa chama hicho, imeendelea kusikilizwa mahakamani, leo tarehe 10 Septemba. Anaripoti Zakia Nanga, Dar es Salaam … (endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mahakama wakati wa kuhairisha shauri hilo, kesi imekuja mahakamani kwa ajili ya kusikiliza ombi la wadai la kutaka kupewa taarifa ya mali za chama hicho.
Kesi hiyo, inasikilizwa na Jaji Hamid Mwanga, katika Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam.
Mbali na Said Issa, wadai wengine kwenye shauri hilo, ni Maulida Anna Komu na Ahmed Rashid Khamis, waliokuwa wajumbe wa bodi ya wadhamini ya Chadema.
- Endelea kufuatilia MwanaHALISI Digital kwa taarifa zaidi.
ZINAZOFANANA
Serikali yamwaga magari mapya kwa Polisi mkoani Mbeya
Lissu: Mahakama hii haina uhalali, Mahakama ya Kisutu imevuruga mchakato
Rais Mwinyi: Ubunifu wa majengo nguzo muhimu katika jamii