August 4, 2025

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Vodacom Corporate Masters yatoa tuzo, zawadi kwa washindi Gofu

 

KAMPUNI ya Vodacom Tanzania, kupitia kitengo cha Vodacom Business kinachoshughulika na wafanyabiashara wakubwa pamoja na wadau mbalimbali wa michezo, wamekabidhi tuzo na zawadi kwa washindi tofauti wa mashindano ya golf yaliyofanyika katika uwanja wa TPDF Lugalo jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hafla hiyo ilikuwa sehemu ya mashindano ya Vodacom Corporate Masters, yaliyolenga kuhamasisha ushiriki wa wadau kutoka sekta mbalimbali kupitia michezo ya kijamii kama golf. Tuzo hizo zilitolewa kwa makundi mbalimbali ikiwa ni pamoja na watoto wa kike na wa kiume, wanawake, wanaume pamoja na wachezaji wa golf waliobobea kutoka mashirika tofauti.

Kupitia tukio hili, Vodacom iliendeleza dhamira yake ya kuunga mkono michezo, kukuza vipaji na kudumisha uhusiano wa kijamii na wadau wake wa karibu.

Mkuu wa Idara ya Masoko na Ushirikiano kutoka Vodacom Tanzania, Joseph Sayi (wa pili kushoto) akimkabidhi tuzo moja ya washindi wa tuzo ya gofu ya kupiga mbali Ali Mamdouhi (wa pili kulia). Tukio hili lilifanyika tarehe 2 Agosti 2025, wakati wa ugawaji wa tuzo uliofanyika na Vodacom Tanzania jijini Dar es Salaam.

About The Author

error: Content is protected !!