
BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya juu (HESLB), imetangaza kufungua dirisha la maombi ya mkopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu. Anaripoti Joyce Ndeki, Dar es Salaam … (endelea).
Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 19 Juni 2025, na Bill Kiwia, Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi hiyo na kusema imetenga Sh. 916.7 bilioni kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu kwa mwaka wa masomo 2025 2026.
Fedha hizo zitawanufaisha jumla ya wanafunzi 99,620 wa mwaka wa kwanza katika ngazi ya za diploma, shahada ya kwanza na shahada za uzamili.
Pia amesema wanafunzi 88000 wa shahada ya kwanza watapangiwa mikopo hiyo.
ZINAZOFANANA
CBE kuendesha kongamano la kuimarisha fursa za ajira
Matokeo mazuri ya kitaaluma Green Acres yaifurahisha serikali
GEL yawanoa wanafunzi wanaokwenda masomoni nje ya nchi