May 15, 2025

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Fainali Simba vs RSB Berkane kupigwa Z’bar

 

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limetangaza kuwa mechi ya pili ya fainali ya kombe la Shirikisho kati ya Simba na RS Berkane ya Morroco itafanyika katika uwanja wa Aman visiwani Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mechi hiyo ilipangwa kufanyika katika uwanja Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam ambao uko kwenye ukarabati.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Caf, Veron Mosengo, imebainisha kuwa uamuzi huo unatokana na ushauri wa kitaalamu waliopatiwa hasa kipindi hiki cha mvua zinazoendelea nchi.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa wanatambua jitihada za serikali na wadau mbalimbali katika kushughulikia ukarabati wa ‘Mkapa’ lakini mechi hiyo itapigwa uwanja wa Aman hivyo waendelee na maandalizi kwenye uwanja huo.

About The Author

error: Content is protected !!