SHIRIKA la Reli Tanzania (TRC) limetangaza kurejea kwa huduma ya ununuzi wa tiketi za treni kupitia mtandao baada ya kukabiliwa na hitilafu ya mfumo wa malipo ya Serikali, maarufu kama Government Electronic Payment Gateway (GePG). Anaripoti Mwandishi Wetu. Dar es Salaam …. (endelea).
Katika taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Habari na Uhusiano wa TRC, Fredy Mwanjala shirika hilo limeeleza kuwa changamoto hiyo ilianza usiku wa kuamkia leo tarehe 5 Aprili 2025 na ilisababisha baadhi ya wasafiri kushindwa kupata namba za malipo (control number) kwa ajili ya kununua tiketi za treni za kisasa (SGR).
“Shirika linaarifu umma kuwa hali ya upatikanaji wa tiketi kwa njia ya mfumo wa GePG imerejea kama kawaida,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.
TRC imetoa pole kwa abiria wote waliokumbwa na usumbufu uliotokana na hitilafu hiyo ya muda mfupi na kuahidi kuendelea kuboresha huduma zake ili kuhakikisha huduma zinapatikana bila vikwazo.
ZINAZOFANANA
Machafuko ya 29 Oktoba: Maaskofu Katoliki wataka wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama wawajibike
Shinikizo la kufanyika uchunguzi wa mauaji ya 29 Oktoba lashika kasi
Meridianbet yaendelea kuwekeza kwa jamii kupitia MRC Rehabilitation Centre