March 9, 2025

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Vodacom, dLab wawezesha wasichana kupitia programu ya CODE LIKE A GIRL

 

KAMPUNI ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na dLab inaendelea kuwawezesha wasichana wenye umri wa miaka 14-18 kwa ujuzi wa STEM kupitia programu ya ‘Code Lie A Girl’. Mpango huu umewawezesha zaidi ya wahitimu 3,000 katika mikoa mbalimbali, ikiwemo Arusha, Dar es Salaam, Mbeya, Dodoma, na Mwanza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hafla ya mahafali iliyofanyika jijini Dar es Salaam iliongozwa na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Vodacom Tanzania Plc, Vivienne Penessis akizungumza na wanafunzi na kuwakabidhi zawadi wahitimu huku akisisitiza dhamira ya Vodacom ya kuwawezesha wasichana kwa ujuzi wa programu (coding) na uvumbuzi.

Programu hii pia inahimiza ujumuishi kwa ushirikishaji wa wasichana wenye ulemavu, ikionyesha azma ya Vodacom ya kuziba pengo la kijinsia katika teknolojia ya kidijitali.

Mkurugenzi wa Raslimali Watu kutoka Vodacom Tanzania Plc, Vivienne Penessis (kushoto) akizungumza na wanafunzi wa programu ya ‘Code Like A Girl’

About The Author

error: Content is protected !!