
KAMPUNI ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na dLab inaendelea kuwawezesha wasichana wenye umri wa miaka 14-18 kwa ujuzi wa STEM kupitia programu ya ‘Code Lie A Girl’. Mpango huu umewawezesha zaidi ya wahitimu 3,000 katika mikoa mbalimbali, ikiwemo Arusha, Dar es Salaam, Mbeya, Dodoma, na Mwanza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Hafla ya mahafali iliyofanyika jijini Dar es Salaam iliongozwa na Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Vodacom Tanzania Plc, Vivienne Penessis akizungumza na wanafunzi na kuwakabidhi zawadi wahitimu huku akisisitiza dhamira ya Vodacom ya kuwawezesha wasichana kwa ujuzi wa programu (coding) na uvumbuzi.
Programu hii pia inahimiza ujumuishi kwa ushirikishaji wa wasichana wenye ulemavu, ikionyesha azma ya Vodacom ya kuziba pengo la kijinsia katika teknolojia ya kidijitali.

ZINAZOFANANA
Nafasi ya kipekee ya kushinda Samsung A25 kwa wapenzi wa kasino
Shinda Samsung A25 bila jasho kwa kucheza Aviator
Meridianbet yaja na Meridian bonanza, ushindi kila mzunguko