March 10, 2025

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Papa Francis atoa kauli yake ya kwanza, awashukuru wanaomuombea

PAPA Francis

PAPA Francis amewashukuru waumini na wasio waumini wa Kanisa Katoliki kwa kuendelea kumuombea afya njema tangu alipolazwa Februari 14,2025. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa, Rome Italia … (endelea).

Papa Francis (88) amelazwa katika Hospitali ya Gemelli mjini Roma akisumbuliwa na maradhi kwenye mfumo wa upumuaji. maradhi hayo yamesababisha asionekane hadharani kwa zaidi ya wiki tatu.

Katika ujumbe wake wa sauti (audio) kwa waumini alioutoa jana jioni  Machi 6,2025, Papa Francis, amesikika akizungumza japo kwa shida. Kauli yake hiyo imeelezwa   kuwarejeshea matumaini waumini wa kanisa hilo ambao wamekuwa wakitumia muda mwingi kumuombea apone.

Hotuba ya Papa Francis, iliyorekodiwa na kutangazwa kupitia vipaza sauti katika uwanja wa Mtakatifu Petro huko Vatican kabla ya sala ya Rozari ya jana jioni, ilikuwa mara ya kwanza kwa wafuasi wake kusikia sauti yake tangu alazwe hospitalini takriban wiki tatu zilizopita.

“Nawashukuru kwa dhati kwa maombi yenu kwa ajili ya afya yangu kutoka uwanjani nami nawasikiliza kutokea hapa hospitalini. Mungu awabariki na Bikira Maria awalinde. Asanteni,” alisema Papa Francis, akizungumza taratibu kwa lugha ya Kihispania ambayo ni lugha yake ya asili.

About The Author

error: Content is protected !!