
RAIS wa Jamhuri ya Muungano Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema uhitaji wa kahawa Duniani ni fursa kubwa Barani Afrika ambako zao hili limegundulika. Anaripoti Apaikunda Mosha, Dar es Salaam … (endelea).
Amezungumza haya katika Mkutano wa tatu wa nchi 25 Barani Afrika, zinazozalisha kahawa (G25 Coffee Summit), amesema takwimu zinaonyesha Dunia nzima watu bilion 3 wanakunywa vikombe vya kahawa kila siku, kati ya hivyo vipo vyenye kahawa nzuri inayozalishwa na wakulima wa Afrika na wengi wao wakiwa ni wakulima wadogo,” amesema Rais Samia.
Amesema kipindi cha nyuma kahawa yetu ilikuwa inaenda ulimwenguni inaongezwa thamani na kurudishwa kwetu na tunauziwa ghali, lakini sasa kumekuwa na ushindani wa uzalishaji na uengezaji wa thamani ya kahawa ndani ya Bara la Afrika.
Rais Samia amesema kuwa hatuna budi kuwapa nguvu vijana wetu ambao ameona wakitengenzeza kahawa pamoja na nakshi ya juu kama inavokuwa ya nchi kama Ujerumani, Uingereza na maeneo mengine, jambo ambalo linaonyesha hatua kubwa ambayo tumeifikia ndani ya Afrika.
Aidha ameeleza ziara aliyofanya mkoani Ruvuma, September mwaka jana alipotembelea shamba la Kampuni ya AVIV, ameona ambavyo uongezaji wa thamani unavoweza kutoa fursa za ajira kwa vijana na wanawake wengi
Hata hivyo amesema kampuni ya AVIV walivutiwa na mazingira mazuri ya uwekezaji hapa nchini na sasa wanalima na kuongeza thamani zaidi ya tani 200 za kahawa ya Arabica na wanaajiri watu zaidi ya 4,000 ikiwemo ajira za msimu wakati wa kupanda na kuvuna.
Mwisho, Rais Samia amesema amefurahishwa kufanyika kwa mkutano huu wa tatu wa nchi zinazozalisha kahawa Barani Afrika, wenye kauli mbiu inayosema “fungua fursa za ajira kwa vijana kupitia uhimarishaji wa kahawa Barani Afrika.”
ZINAZOFANANA
Vodacom Foundation kufadhili kongamano la Utafiti wa Elimu Tanzania 2025
ACT Wazalendo wajifungia kujadili Uchaguzi Mkuu 2025
SBL yazindua kampeni ya SMASHED kukabiliana na unywaji wa pombe chini ya umri