
MWANAHARAKATI Maria Sarungi raia wa Tanzania, ametekwa nyara nchini Kenya na watu wenye silaha kali na kutokomea nae kusiko julikana. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kenya … (endelea).
Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International linasema kwamba mwanaharakati na mhariri wa kujitegemea kutoka Tanzania Maria Sarungi ametekwa nyara akiwa nchini Kenya.
Katika taarifa kupitia mtandao wa X, shirika hilo limesema kwamba Maria alitekwa na wanaume watatu waliokuwa na silaha na ambao walikuwa na gari nyeusi aina ya Noah.
Aidha limeongeza kuwa kisa hicho kimetokea mwendo wa saa tisa na robo mchana katika eneo la Chaka Place, mtaa wa Kilimani mjini Nairobi.
Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo Irungu Houghton ameiambia BBC kuwa wako katika eneo la tukio wakijaribu kupata taarifa zaidi.
ZINAZOFANANA
Julai 11 Mahakama kuamua mapingamizi ya Serikali kesi Lissu
SBL yakabidhi mradi wa maji kwa wakazi 14,000 Kwadelo, Kondoa
Meridianbet yaigusa hospitali ya Palestina Sinza