JESHI la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam, linamshikilia kwa mahojiano aliyekuwa balozi wa Tanzania nchini Sweeden, Dk Willibrod Slaa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Slaa alikamatwa jana usiku nyumbani kwake Bweni na mpaka sasa Jeshi hilo halijaweka wazi tuhuma zinazomkabili mwanasiasa huyo ambaye pia amepata kuhudumu katika wadhifa wa Katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na mbunge wa Karatu.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, mahojiano na mwanasiasa huyo yamekwenda vizuri na hivi sasa wanaangalia sheria zinasemaje ili wachukue hatua zaidi.
Hata hivyo kamanda Muliro hakuwa tayari kueleza kwa undani tuhuma zinazomkabili Dk Slaa ambaye amekuwa mkosoaji mkubwa wa serikali na viongozi wake.
ZINAZOFANANA
Wakili Mahinyila Mwenyekiti mpya Bavicha
TMA yatoa taarifa ya uwepo wa Kimbunga Dikeledi, pwani ya Msumbiji
Bashungwa azuiwa vitambulisho 31,000 vya NIDA