September 19, 2024

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Jubilee Insurance yazindua kampeni ya ‘Kuna kuishi, na Kuna kuishi Huru’

Mtendaji Mkuu wa Bima ya Maisha ya Jubilee, Helena Mzena (kulia)

 

KAMPUNI ya Jubilee Insurance imezindua kampeni kabambe iliyopewa jina la ‘Kuna kuishi, na Kuna kuishi Huru’, inayolenga kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa bima kwa maisha ya kila siku. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kampeni hiyo ambayo itakuwa endelevu, haitakuwa kwa wananchi wa Tanzania pekee bali itawagusa majirani wa Kenya na Uganda.

Mtendaji Mkuu wa Bima ya Maisha ya Jubilee, Helena Mzena amesema mpango huo utakutana na watu binafsi katika maeneo yao ya mahitaji kwa kuimarisha uelewa wao wa uwekezaji na ufumbuzi wa bima.

Alisema kwa kufanya hivyo, kampuni itawapa uwezo wa kufanya maamuzi sahihi ambayo yanalinda mustakabali wao wa kifedha na kuchangia utulivu wa muda mrefu.

Helena alisema uelewa wa umuhimu wa bima upo chini katika ukwanda wa Afrika Mashariki tofauti na kanda nyingine hivyo elimu wanayolenga kuitoa itasaidia wananchi kufanya maamuzi ya kuingia katikamfuko wa bima.

“Lengo letu kubwa ni kuelimisha jamii juu ya umhimu wa kuwa na bima ili kumfanya aishi maisha ambao yana uhuru kwa maana lolote litakalotokea atakuwa na uwezo wa kukabiliana nalo kwa kuwa ana bima,” alisema Helena.

Helena alisema Watanzania wanaotumia huduma ya bima wapo 1% hivyo kupitia kampeni hii wataongeza uelewa ambao utawafanya kuchukua maamuzi sahihi ya kujiunga na huduma hiyo.

“Kwa zaidi ya miaka 87 ya uzoefu wa kutoa hudumayabima, tunajitolea kutoa elimu ambayo lengo lake ni kurahisisha maisha ya wateja wetu na jamii kwa ujumla,” amesema Helena.

Mtendaji Mkuu wa Bima ya Afya ya Jubilee, Dk. Harold Adamson (kushoto)

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa Bima ya Afya ya Jubilee, Dk. Harold Adamson amesema kampeni hiyo inaenda kuondoa dhana kuwa watumiani wa bima ni watu wenye kipato cha juu na waajiriwa hasa serikalini kwa kutoa elimu sahihi kwa matumizi ya bima.

Dk. Harold amesema mpango wetu huu mpya unaonyesha dhamira yetu ya kwenda zaidi ya jukumu lao la kawaida la kutoa huduma ya bima.

“Hatutoi huduma tu; tunashiriki maarifa muhimu ambayo yatawasaidia watu kufanya chaguo bora kwa afya zao. Lengo ni kuleta mabadiliko ya kweli katika maisha ya wale tunaowahudumia,” amesema Dk. Harold.

Kama Ripoti ya Mtazamo wa Bima ya 2023 ya Deloitte inavyoonyesha, kupenya kwa bima nchini Tanzania, Uganda na Kenya ni chini ya 2% ya Pato la Taifa.

Hii inaangazia pengo dhahiri katika chanjo. Ripoti ya Global Findex pia inaonyesha kuwa ni 41% tu ya watu wazima katika nchi hizi wana uwezo wa kifedha. Hii ina maana kwamba chini ya nusu ya watu wako tayari kushughulikia curveballs za kifedha.

Kampeni ya “Kuna Kuishi, na Kuna Kuishi Bila Malipo” itawapa watu binafsi ujuzi wa kufanya maamuzi sahihi ambayo yanakuza ukuaji wa mali huku wakifikia malengo yao ya kifedha na kulinda afya zao.

About The Author