
Leo, katika kusikilizwa kwa kesi ya mwandishi wa habari Eric Kabendera katika Mahakama Kuu ya Tanzania, ambapo amewasilisha kesi ya fidia ya dola milioni 10 dhidi ya Vodacom, kampuni hiyo imekanusha vikali madai hayo.
Akizungumza na vyombo vya habari, Mtaalamu Mwandamizi wa Sheria kutoka Vodacom, Joseph Tungaraza alisema, “Tunakanusha vikali madai ya mlalamikaji. Tunatoa huduma zetu kwa wateja wetu wote kwa kuchukua hatua madhubuti za faragha ya data. Kulinda usiri na usalama wa data zote ni jambo muhimu, na tunaendelea kutekeleza taratibu zote za kisheria za kulinda taarifa nyeti za wateja ila kuhakikisha uaminifu na faragha ya wadau wetu kwa ujumla unabakia kuwa kipaumbele chetu.
“Tunakataa madai ya mlalamikaji, tunatoa huduma zetu kwa wateja wote kwa kujitolea kwa dhati kwa hatua thabiti za usiri wa data. Kulinda usiri na usalama wa data zote ni jambo la msingi, na tunaendelea kutekeleza taratibu kali za kulinda taarifa nyeti, kuhakikisha kuwa imani na faragha ya wadau wetu inabaki kuwa kipaumbele chetu cha kwanza – Joseph Tungaraza, Senior Legal Specialist Vodacom
ZINAZOFANANA
Tata yaja na mpango wa kusafirisha mizigo mikubwa, wakulima watajwa kunufaika
NBC yaitambulisha “NBC Shambani’’ kwa wakulima wa Ufuta Pwani
Meridianbet yazindua “GIFT WEDNESDAY” shinda Samsung A25 mpya kila wiki