RAIS wa Uganda, Yoweri Museveni anatarajiwa kuwasili nchini kesho Jumamosi 7 Februari 2026, kwa ziara ya kikazi ya siku moja. Anaripoti Zakia Nanga, Dar es Salaam … (endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Ijumaa 6 Februari 2026 na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, imesema Rais Museveni atafanya mazungumzo na mwenyeji wake, Rais Samia Suluhu Hassan, yakilenga kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na ushirikiano wa kiuchumi kati ya nchi hizo mbili.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa miongoni mwa ajenda kuu za mazungumzo hayo ni masuala ya nishati, hususan Mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), unaotarajiwa kuleta manufaa kwa Tanzania, Uganda na ukanda wa Afrika Mashariki kwa ujumla.
Viongozi hao wawili pia wanatarajiwa kujadili masuala mbalimbali ya kikanda na kimataifa yanayogusa maslahi ya pande zote mbili, ikiwemo biashara, usalama na miundombinu.
ZINAZOFANANA
Spika aitaka Serikali iweke maeneo ya kihistoria ya Papa Leo XIV
7 wajishindia TV na Bajaji kupitia kampeni ya “Mwaka Umenyooka na Myairtelapp”
TAMISA yawahamasisha vijana kuchangamkia fursa za uwekezaji katika sekta ya madini